
Wafanyakazi
wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), leo wamepata mafunzo ya kukabiliana na
majanga, hasa janga la moto, mafunzo yaliyo endeshwa na wafanyakazi wa NDC,
Sadick Nembo pamoja na Robert William, zoezi lililo fanyika kwenye ofisi za
NDC, Posta, jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi
hao walifundishwa aina za mioto, namna ya kujikinga, tahadhari za kuchukua ili
kuepukana na moto, pamoja na namna ya kukabiliana na moto pindi unapotokea. Mbali
na hivyo, wafanyakazi wa NDC walifundishwa namna ya kutumia na kutunza vifaa
vya umeme wawapo kazini au nyumbani ili kuhakikisha wanazuia matukio yanayoweza
kusababishwa na moto.
Wafanyakazi wa NDC wakifundishwa namna ya kukabiliana na moto wawapo kazini au nyumbani.
“Leo wafanyakazi wa NDC wamefundishwa namna ya
kukabiliana na moto pindi unapotokea, na elimu hii itawasaidia wawapo kazini au
nyumbani,” ameeleza Robert William, mkufunzi wa zoezi hilo.
Aliendelea
kueleza kuwa janga la moto linaweza kuzuiwa kwa kutumia vizuri vifaa ya umeme kwa
kuhakikisha vinazimwa pale ambapo havitumiki na kuvikagua mara kwa mara. “Unapomaliza
shughuli zako ni vyema ukazima taa au swichi ya umeme.”
Pia,
wafanyakazi hao wameoneshwa maeneo wanayoweza kukimbilia pindi moto unapotokea (Assembly
point), pamoja na vifaa wanavyoweza kuvitumia moto unapotokea kazini.
“Pale
moto unapotokea unaweza kutumia vizima moto (fire extinguisher), mchanga
au kama moto bado upo hatua za awali unaweza kutumia kitambaa kizito kuuzima,”
amee;eza Sadick Nembo, mkufunzi wa zoezi hilo.
Sambamba
na hilo amewaasa wafanyakazi wa NDC pamoja na umma kutohamaki pale moto
unapotokea bali wawe watulivu ili kuipa akili kuweza kufanya maamuzi sahihi
ikiwemo kutafuna mbinu za kuzima moto husika na kuwaita Jeshi la Zima Moto na Uokoaji.
Mafunzo
haya ni sehemu ya kuwajengea ujuzi wafanyakazi wa NDC ambapo hufundishwa stadi
mbalimbali zikiwemo; uchumi, maisha ya kazi na nje ya kazi, biashara, afya na
mambo mengine mengi.