Shirika la Taifa la Maendeleo ni taasisi ya umma iliyoanzishwa kwa
mujibu wa tangazo la Serikali, the
National Development Corporation (Establishment) Order, G.N. No. 90 of 1969.
Shirika hili limeendelea kuwepo chini ya Sheria ya Mashirika ya Umma, Sura Na.
257 ya mwaka 2002. Jukumu kubwa la Shirika ni kuendeleza na kutekeleza miradi
ya kiuchumi kwa kushirikiana na sekta binafsi. Baadhi ya majukumu ya Shirika ni
kama yafuatayo: -
(a)
Kuanzisha, kuendeleza na kusimamia viwanda vya
msingi nchini likishirikiana na sekta binafsi na wadau wengine wa ndani na nje
ya nchi.
(b)
Kuchangia kasi ya mabadiliko ya mfumo wa uzalishaji
nchini kwa kuanzisha na kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa mipya, na yenye
uhusiano mkubwa na sekta/shughuli asilia za wananchi.
(c)
Kusaidia ushiriki wa wananchi wengi katika shughuli
za kiuchumi; hii ikiwa ni pamoja na kusaidia upatikanaji wa miundombinu na
kubuni mifumo ya kisasa inayokubalika kwa uendeshaji wa biashara.
(d)
Kulinda maslahi ya nchi kwa
kumiliki hisa katika miradi mikubwa na ya kimataifa, ili hatimaye kutoa fursa
kwa wananchi wazawa kuzinunua na kumiliki na hivyo kuendesha uchumi rasmi na biashara za kimataifa;
(e)
Kuishauri
Serikali kwenye mambo yanayohusu mendeleo ya viwanda pamoja na sera na mipango mikakati yake.