RAIS AMTEUA DKT. SHOMBE KUWA MKURUGENZI MWENDESHAJI NDC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dkt. Nicolaus Herman Shombe kuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC).

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Shombe alikuwa Kamishna wa Mipango, Wizara ya Fedha na Mipango. Dkt. Shombe anachukua nafasi ya marehemu, Prof. Damian Gabagambi.

Uteuzi huo umeanza tarehe 29 Oktoba, 2021.